Skip to main content

Posts

Showing posts from August 21, 2017

TATIZO LA NGUVU ZA KIUME.

Zifahamu Nutrients na madini muhimu kwa Nguvu za Kiume. Siku hizi wanaume wengi wamekumbwa na tatizo la ukosefu wa nguvu za kiume kwa maana ya kutokuwa na uwezo wa kusimamisha uume wakati wa kufanya mapenzi, kushindwa kuendelea kusimamisha hadi mwisho wa tendo na kushindwa kurudia tendo hadi kuwaridhisha wenzi wao. Kadhalika wengine wamekuwa na tatizo la mbegu zao za kiume kutokuwa na umbile bora (sperm abnormalities) linaloziwezesha kusafiri kwa kasi ya kutosha katika uke wa mwanamke (sperm motility). Aidha wengine shahawa zao zina mbegu kidogo (low sperm count). Mwanaume anapomwaga shahawa wakati wa kufanya mapenzi shahawa hizo hupaswa kuwa na mbegu za kiume kiasi cha milioni 50 kwa kila milimita moja ya shahawa. Endapo kiasi hicho kitapungua chini ya miioni 20 uwezo wa uzazi (fertility) wa mwanaume huwa na kasoro. Matatizo yote hayo yanatokana na wanaunaume wengi kutokula vyakula sahihi au ulaji wa vyakula hivyo kwa kiwango kidogo ikilinganishwa na mahitaji ya m...

NAMNA YA KUONDOA TATIZO LA KUPATA CHOO KIGUMU.

Kwanza kabisa matatizo tajwa hapo hayana sababu Ya moja kwa moja bila ya kupata vipimo vya kitaalam kugundua tatizo Ni nini ktk mfumo mzima wa umeng'enyaji wa chakula lkn hudhaniwa kuwa upungufu wa maji ktk umeng'enyaji wa chakula, uhaba wa vyakula vyenye nyuzi nyuzi (Fiber food), uwingi wa vyakula vya protein mfano Mayai n.k hupelekea matatizo hayo tajwa..... Tatizo hili laweza kukuondoka bila shaka ukizingatia yafuatayo (Diet na matibabu asilia) BiidhniAllah.... DIET Ktk diet yakupasa kuviendea vyakula na matatunda yenye Asili ya nyuzi nyizi na mfano wa vyakula na matunda hayo Ni kama ifuatavyo VYAKULA ♻ Brown rice (wali wa brown) ♻ whole wheat bread/Brown Bread (Mkate wa Brown) ♻ White Beans (maharage meupe) ♻ Black Beans (Maharage meusi) ♻ Oats meals (zapatikana Sanaa supermarket) ♻ Broccolis ♻ pumpkin (Maboga) ♻ viazi vitamu (chemsha na maganda yake ule hivyo hivyo usitoe kitu) ♻ Tende ♻ na jamii zinginezo za vyakula vya ngano MATUNDA ♻ Apples (red a...

TATIZO LA MENINJITISI

Ni inflamesheni ya tando zinazofunika na kuukinga ubongo na uti wa mgongo , sehemu inayojulikana kwa kijumla kama meninjesi. Inflamisheni hii inaweza kusababishwa na maambukizi ya virusi,bakteria,au na vimelea wengine. (Inflamisheni humaanisha  maumivu.) Dalili za meninjitisi zinazotokea mara nyingi ni maumivu ya kichwa na kukazika kwa shingo , hali inayohusishwa na homa , kuchanganyikiwa au ufahamu uliogeuka, kutapika, na kukosa uwezo wa kustahimili mwanga (fotofobia ) au kelele kali ( fonofobia ). Mara nyingi watoto hudhihirisha dalili zisizo mahususi pekee kama vile kizunguzungu na kuwashwa. Uwepo waupele unaweza kuwa dalili ya kisababishi maalumu cha meninjitisi; kwa mfano, meninjitisi inayosababishwa na bakteria aina ya meningokokasi unaweza kuambatana na upele. Kwa watu wazima, dalili ya meninjitisi inayotokea mara nyingi ni maumivu ya kichwa yaliyo makali, ambayo hutokea kwa karibu asilimia 90 ya visa vya meninjitisi ya kibakteria,ambavyo hufuatwa na ku...

UGONJWA WA STROKE ( KIHARUSI )

UGONJWA WA STROKE(KIHARUSI) Fahamu aina za kiharusi(strocke). Kiharusi au kwa Kiingereza Stroke ni kitendo cha baadhi ya viungo vya mwili kuwa na ganzi au kutojiweza kufanya kazi zake za kawaida. Kuna aina mbili za kiharusi, lakini kabla ya kuchambua hayo tuangalie,ni nini kinasababisha mtu kukumbwa na ugonjwa huu ?. Mtu anaweza kupata dalili za ugonjwa huu wa kiharusi na baada ya dakika chake zikaisha. Kiharusi kinampata binadamu baada ya eneo la ubongo kukosa damu kwa saa 24 ama zaidi au kunapotokea kizuizi cha damu au mishipa ya damu kushindwa kusafirisha damu au mshipa huo unapopasuka. Kiharusi kimegawanyika katika aina kuu mbili kulingana na jinsi kinavyotokea. kwanza ni: 1.Kiharusi cha kukosa hewa kwenye ubongo kitaalamu huitwa Ischemic stroke. (Ischemic ni neno la Kigiriki lenye maana ya kuzuia damu). Aina hii ya kiharusi hutokea iwapo usambazaji wa damu katika sehemu ya ubongo hupungua na kusababisha tishu za ubongo za eneo lililoathirika kushin...

SARATANI YA NGOZI

UGONJWA WA SARATANI YA kwa undani kuhusu saratani ya ngozi iitwayo Melanoma kwani saratani si tu kwamba ni ugonjwa hatari lakini pia ni ugonjwa unaompa mwanadamu mateso makali kutokana na maumivu anayoyapata. Maumivu hayo huyapata mgonjwa bila kujali kama anaugua saratani ya ngozi, ya mifupa, damu, tumbo au ya kizazi. Shida ya maradhi haya ni kwamba matibabu yake yanahitaji gharama kubwa mno. Melanoma ni saratani ya hatari sana kwa maisha ya mwanadamu inapotokea mtu akaipata, basi maisha yake yanakuwa hatarini. Saratani hii si rahisi kuigundua ukilinganisha na saratani nyingine za ngozi lakini pia husambaa haraka zaidi mwilini kuliko saratani nyingine za ngozi. Melanoma huweza kusambaa na kushambulia viungo vingine zaidi ya ngozi kama mifupa na ubongo. Inapofikia hatua hii saratani hii inakuwa ngumu sana kutibika. Dalili. Dalili za saratani hii zipo nyingi na ni vema kila mtu afahamu, mojawapo ni kubadilika kwa ukubwa, rangi au ule muundo wa alama ya ngozi ...