Skip to main content

Posts

Showing posts from September 23, 2017
KUNG'ARISHA USO NA KUTOA MADOA DOA USONI. Chukua uwatu usage mpaka uwe laini sana. Kisha utaosha uso wako kwa maji vuguvugu na ukaushe kabisa. Baada ya hapo utachukua unga wa uwatu kijiko kimoja na utachanganya maji ya kawaida ama maji ya waridi mpaka iwe marham/rojo (paste) na utajipaka usoni na kuiacha ikauke kwa mda wa dakika 10-15 na utaosha na kupaka mafuta yako. NB Hakikisha zoezi hili unalifanya mara tatu kwa wiki kwa ajili ya matokeo mazuri. Na ni bora ukifanya usiku kabla hujalala.
NAMNA YA KUTENGENEZA SIKI YA APPLE. Mahitaji - apple mbili - Kopo lililo na mfuniko. - sukari - maji Matayarishi Unachukua apple unazikatakata vipande vidogo vidogo, kisha unavitia ndani ya lile kopo kisha unatia maji kwenye lile kopo na kuweka sukari hakikisha glass moja ya maji kwa sukari kijiko kimoja, tia maji kwenye kopo Baada ya hapo funika na na uhifadhi sehemu salama. Hakikisha unakoroga kila baada ya siku kadhaa. Utaacha kwa mda wa siku 14. Kisha chuja na hifadhi kwenye friji ili ikae mda mrefu. Baada ya mda kuisha itakuwa siki tayari na unaweza kuijaribu kwa kuionja ama kusikiliza harufu yake. Siki mara nyingi inatumiwa kama dawa, kiungo katika kupikia ama kusafishia vyombo.