Skip to main content

Posts

Showing posts from October 24, 2017

BUNSAJI

Leo nataka kupeana faida ndogo kuhusu mafuta yaliyochanganywa na *BUNSAJI.*mafuta haya hufaa sana kwa :- - kichwa kilicho na harara ukipaka kichwani. - mafuta hayo huwafaa sana watu ambao hawapati usingizi wakipaka kichwani. - mafuta hayo hurutubisha ubongo ukipaka kichwani. - hufaa sana kwa watu wenye uyabisi na kupasuka pasuka ( dandruff ) ukipaka kichwani. -  hufaa sana kwa mtu anaejikuna sana kichwani.  *NAMNA YA KUYATENGENEZA.* chukua bunsaji kisha iponde iwe unga kisha iroweke katika maji unayotaka kuyachemsha masaa 12, baada ya hapo utaichemsha sana mpaka ibaki sawa na mafuta yako unayotaka kuchanganyia kama ni ya nazi, zaituni ama yeyote yale. Kama itakuwa mafuta yako ni nusu lita hakikisha umeichemsha bunsaji mpaka ikafika nusu lita nayo, kisha changanya pamoja baada ya kuichuja na uweke jikoni ichemke mpaka maji yote ya bunsaji yamekauka na kubaki mafuta pekee. Hapo sasa itakuwa tayari kwa matumizi. Kwa ushauri/tiba ya maradhi mbalimbali wasiliana nami.

ALMONDS/LOZI

leo ndugu zangu nataka kuzungumzia faidia cheche zitokanazo na tunda hili. watu wengi wamelichukulia tunda hili huliwa na watu wenye maradhi ama wenye hela zao. Ila kwa ushauri nawaomba tukumbatie tunda hili kwa wingi maana lina faida nyingi sana. Hizi ni baadhi ya faida ya tunda hili:- - husafisha tumbo. - huongeza maziwa mengi kwa wanyonyeshaji. - kusaidia sana kwa wenye maradhi ya mishipa/nerves. - husaidia sana kwa watu wenye maradhi ya kibofu cha mkojo. - lozi ni nzuri sana kwa mtu mwenye maradhi ya figo. - ni nzuri sana kwa wenye maradhi ya kisukari. - hufungua njia za mkojo. - lozi hutia nguvu ubongo hasa kwa wenye kusahau sahau na udhaifu wa kumbukumbu. - mafuta yake ni mazuri kwa mtu mwenye maradhi ya ngozi hutibu. - mafuta yake ni mazuri kwa mtu aliepooza, hutibu. - mafuta yake ni mazuri kwa mtu aliyechomeka ngozi, hutibu. - lozi husaidia kwa mtu mwenye uchache wa mbegu za kiume. NB tunda hili linatibu maradhi mengi sana. Kwa ushauri/tiba wasiliana nami...