Skip to main content

ALMONDS/LOZI


leo ndugu zangu nataka kuzungumzia faidia cheche zitokanazo na tunda hili.
watu wengi wamelichukulia tunda hili huliwa na watu wenye maradhi ama wenye hela zao. Ila kwa ushauri nawaomba tukumbatie tunda hili kwa wingi maana lina faida nyingi sana. Hizi ni baadhi ya faida ya tunda hili:-

- husafisha tumbo.
- huongeza maziwa mengi kwa wanyonyeshaji.
- kusaidia sana kwa wenye maradhi ya mishipa/nerves.
- husaidia sana kwa watu wenye maradhi ya kibofu cha mkojo.
- lozi ni nzuri sana kwa mtu mwenye maradhi ya figo.
- ni nzuri sana kwa wenye maradhi ya kisukari.
- hufungua njia za mkojo.
- lozi hutia nguvu ubongo hasa kwa wenye kusahau sahau na udhaifu wa kumbukumbu.
- mafuta yake ni mazuri kwa mtu mwenye maradhi ya ngozi hutibu.
- mafuta yake ni mazuri kwa mtu aliepooza, hutibu.
- mafuta yake ni mazuri kwa mtu aliyechomeka ngozi, hutibu.
- lozi husaidia kwa mtu mwenye uchache wa mbegu za kiume.

NB tunda hili linatibu maradhi mengi sana.

Kwa ushauri/tiba wasiliana nami
karibuni mombasa kenya

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA MTU ALIEINGIWA NA JINNI SUGU.

kabla sijatoa tiba yake, ni lazima ujue unatibu nini na kwanini ni jinni. Maana zipo dalili mbalimbali zinazoonyesha mgonjwa amehusudiwa na jini na ni jini aina gani aliemuingilia muhusika. Zifuatazo ni aina na utaratibu wa kumtibu jini sugu. Dawa za kula. Habbatsaudai Habbatsufa Bakahadi Manimani Uzile Habbat rehani Karkam Halilinji Alhamza Kamun aswad Zamda Khardal Daarfilfil Filfil aswad Haltit Zaatar Harmal Sufa nyeupe Manimani Shomari Udinadi Ulinjani Sakabanji Kamun abyadh Uwatu Giligilani Karafuu Tangawizi Mdalasini Maua waridi Hakikisha dawa hizi umezitwanga na kuwa laini kisha utachukua kijiko kimoja cha kila dawa na kuchanganya kwenye asali safi ya nyuki lita moja na uisomee ruqya na mgonjwa awe anakunywa vijiko viwili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 30. NB Hakikisha wakati mgonjwa anatumia dawa za kula ambatanishe na za kujifukiza pamoja na za kujipaka. DAWA ZA KUFUKIZA kiribiti upele Sandarusi Haltit Karafuu maiti Mruturutu ...

KUONDOSHA MARADHI YA SUBIAN NA KUONDOA WASIWASI

Kwa mtu mwenye matatizo hayo achukue dawa zifuatazo :- - unga wa ambari nyeusi. - unga wa mvuje. - unga wa kitunguu thaum. - mafuta ya uto. - mafuta original ya zaituni. Maelezo Changanya na iwe unajipaka mwili mzima asubuhi na jioni kwa mda wa siku 21.

UTOSI KUINGIA NDANI KWA MTOTO MCHANGA.

chukua manjano mbichi iponde iwe laini sana, kisha chukua pamba na uiweke ile dawa, kisha muekee mtoto mchanga aliena tatizo hilo utosini. In shaa allah utosi utarudi sawa. Utafanya hivyo kwa siku mara moja mpaka tatizo litakapokwisha.