Skip to main content

Posts

Showing posts from August 19, 2017

KUONDOSHA MARADHI YA SUBIAN NA KUONDOA WASIWASI

Kwa mtu mwenye matatizo hayo achukue dawa zifuatazo :- - unga wa ambari nyeusi. - unga wa mvuje. - unga wa kitunguu thaum. - mafuta ya uto. - mafuta original ya zaituni. Maelezo Changanya na iwe unajipaka mwili mzima asubuhi na jioni kwa mda wa siku 21.

KUFA GANZI - PERIPHERICAL NEUROPATHY

Chukua - Kamun aswad - Haltit - Hardal - Manjano - Kungumanga - Mafuta ya habbat soda. Hakikisha dawa hizo ziwe ujazo sawa isipokuwa mafuta ya habbatsoda yazidi kidogo changanya na mpake mgonjwa sehemu husika kwa kutumia pamba.

HOMA YA MATUMBO

Homa ya matumbo Homa ya matumbo  husababishwa na bakteria anayeitwa  Salmonella  Typhi . Ugonjwa huu huambukizwa kwa mtu kula au kunywa chakula au maji yalio na kinyesi cha mu aliyambukizwa. [1] Bakteria hawa hutoboa na kunyonya chakula kwenye matumbo ya binadamu Tiba Chukua unga wa uwatu na unga wa sanamaki na uchanganye pamoja kwa ujazo sawa na iwe mgonjwa anatia kijiko kimoja kikubwa kwa uji mwepesi usio na sukari asubuhi na jioni kwa mda wa siku 11.

PARACHICHI

Faida za parachichi. Parachichi ni tunda ambalo mti wake hujulikana kisayansi kama Persea amerikana. Tunda hili lina aminika kuwa na asili kutoka jimbo la Puebla,bara Amerika ya kusini kunako nchi ya Mexico. Lakini kutokana na faida nyingi kiafya zipatikanazo kwa ulaji wa tunda hili, tunda hili sasa hupatikana na kutumika kwa lishe sehemu nyingi duniani hususani barani Afrika. Parachichi ni tunda la pekee ukilinganisha na matunda mengine, kimsingi matunda mengine huwa yana wanga( carbohydrate) kwa wingi,wakati parachichi lina aina ya mafuta ambayo yana faida kwa afya. Parachichi katika tafiti nyingi limeonekana kuwa na faida katika afya ya moyo. Wagonjwa wa moyo wamekuwa katika makatazo ya kutumia aina ya mafuta ambayo yamekuwa yakichangia kuongezeka kwa lehemu katika damu(mafuta hayo kitaalam kama polysaturated fat ), na kuongeza matumizi ya mafuta yasiyoongeza lehemu katika damu (monosaturated fat ). Parachichi ni chanzo kizuri cha mafuta yasiyoongeza lehemu kati...

MENO KUUMA, KUTOBOKA, KUOZA, KUVIMBA UFIZI NA KUTOA HARUFU KINYWANI.

kwa mtu mwenye matatizo hayo basi achukue dawa zifuatazo:- - unga wa pilipili manga. - karafuu - shabu Maelezo Hakikisha kila moja iko hali ya unga na utachanganya zote kwa pamoja kwa ujazo sawa. Na utakuwa unapigia mswaki baada ya kupiga mswaki kwa mda wa dakika zisizopungua 5, mara mbili kwa siku mpaka utakapo poa.

MABUSHA

Kwa undani kuhusu mabusha. Mabusha ni hali ya kujaa maji kwenye mfuko wa pumbu. Hali hii hutokea kunapokuwa na mkusanyiko wa maji kati ya tabaka mbili za utando unaozunguka korodani. Dalili za Mabusha. Katika hatua za awali, mabusha hayana dalili zozote (asymptomatic). Hata hivyo, baada ya muda fulani, mapumbu hujaa na uvimbe huweza kuonekana hata kwa nje. Kwa kadiri uvimbe unavyozidi kuongezeka, dalili zifuatazo zaweza kujitokeza pia; Muhusika kujihisi hali ya uzito na kuvuta sehemu za siri kutokana na kujaa na kuongezeka kwa uzito wa mapumbu. Mgonjwa huweza kujihisi hali ya usumbufu na kutojisikia vizuri maeneo ya kinena mpaka mgongoni. Kwa kawaida mabusha hayana maumivu yeyote. Hata hivyo, iwapo mgonjwa ataanza kujihisi maumivu, hiyo ni dalili ya kuwepo kwa uambukizi katika mshipa wa epididymis (acute epididymitis). Uvimbe huwa na tabia ya kupungua iwapo mgonjwa atakaa kitako na huongezeka pindi anaposimama. Iwapo mgonjwa atajisikia homa, kichefuche...

UGONJWA WA INI

Chukua binzari shomari robo kilo na uisage mpaka iwe laini sana na mgonjwa atumie kijiko kimoja cha chakula kwa maji ya moto kutwa mara tatu kwa mda wa siku 30.