Skip to main content

PARACHICHI

Faida za parachichi.

Parachichi ni tunda ambalo mti wake hujulikana kisayansi kama Persea amerikana.

Tunda hili lina aminika kuwa na asili kutoka jimbo la Puebla,bara Amerika ya kusini kunako nchi ya
Mexico.

Lakini kutokana na faida nyingi kiafya zipatikanazo kwa ulaji wa tunda hili, tunda hili sasa hupatikana na kutumika kwa lishe sehemu nyingi duniani hususani barani Afrika.

Parachichi ni tunda la pekee
ukilinganisha na matunda mengine,
kimsingi matunda mengine huwa yana wanga( carbohydrate) kwa wingi,wakati parachichi lina aina ya mafuta ambayo yana faida kwa afya.

Parachichi katika tafiti nyingi
limeonekana kuwa na faida katika
afya ya moyo. Wagonjwa wa moyo
wamekuwa katika makatazo ya
kutumia aina ya mafuta ambayo
yamekuwa yakichangia kuongezeka
kwa lehemu katika damu(mafuta hayo kitaalam kama polysaturated fat ), na kuongeza matumizi ya mafuta yasiyoongeza lehemu katika damu (monosaturated fat ).

Parachichi ni chanzo kizuri cha mafuta yasiyoongeza lehemu katika damu.

Utafiti unaonyesha kuwa matumizi ya mafuta haya katika parachichi
hupunguza lehemu iliyo hatari
( kitaalam kama, Low density
lipoprotein ), na huchangia katika
ongezeko la lehemu isiyo hatari
( High density lipoprotein ).

Madini ya Potasiamu ni aina ambayo
huwa watu hawapati ya kutosha
kutoka katika vyakula. Parachichi lina kiwango kikubwa cha madini ya potassium kuliko ndizi. Tafiti
mbalimbali zimeonyesha kuwa
matumizi ya madini haya huambatana na kupungua kwa shinikizo la damu,

shinikizo la juu la damu laweza
kupelekea mtu kupata kiharusi,
shambulizi la moyo hata figo
kushindwa kufanya kazi.

Parachichi lina kiwango kikubwa cha fiba. Fiba ni kirutubisho kutoka katika vyakula vya jamii ya mimea, fiba huwa hazimeng’enywi tumboni lakini huwa zina umuhimu mkubwa sana, kama kusaidia kupunguza uzito wa mwili, kusaidia urekebishaji wa kiwango cha
sukari mwilini na kupunguza hatari ya kupata magonjwa mengi mwilini.

 Kuna aina fulani ya fiba ambazo huwa ni virutubisho kwa ajili ya bakteria wenye faida tumboni, hii huimarisha kinga ya mwili na kusaidia mwili kufanya kazi
katika kiwango kinachotakiwa.Kwa
kuwa parachichi lina kiwango kikubwa cha fiba, husaidia kuboresha mmeng’enyo na kupata choo katika hali ya kawaida.

Aina ya mafuta na virutubisho
tulivyoviona awali katika parachichi
vinasaidia afya ya ngozi yako.

Husaidia ngozi yako kutokuwa kavu
na kuwa na unyevu unaotakiwa na
kuifanya ngozi kuwa laini na yenye
afya.

Vitamini C husaidia katika kusaidia uponaji haraka wa ngozi na
kujijenga upya kwa seli za ngozi
zilizoharibika,husaidia kujenga elastini na collageni ambazo ni muhimu katika ngozi. Uwepo wa virutubisho viondoavyo sumu
( antioxidants) katika parachichi kama carotenoidi na vitamini E, hutusaidia kutukinga na
mionzi mikali ya jua, kwa hiyo huzuia makunyanzi katika ngozi na kuifanya ngozi yako kuwa na mwonekano mzuri wakati wote.

Tunda hili ni lishe bora kwa wale
wenye kisukari. Parachichi lina
kiwango kidogo cha sukari
ukilinganisha na matunda mengine.

Pia uwepo wa mafuta aina ya
‘monosaturated’ husaidia kuboresha
ufanyaji kazi wa homoni ya insulini,
katika urekebishaji wa kiwango cha
sukari mwilini.

Faida nyingine ni kuwa Vitamini C katika parachichi husaidia kuimarisha mishipa ya damu na kuboresha kinga ya mwili ambayo ni faida kubwa kwa wagonjwa wenye kisukari.

Faida katika afya ya uzazi ni dhahiri. Parachichi lina Vitamini E ambayo ni “antioxidant ” Potasiamu, Vitamini B6,Vitamini C ambazo hutusaidia kutukinga na magonjwa ya moyo hata yale ya kisukari.

Chochote kile kinachosaidia afya ya moyo pia husaidia afya ya uzazi.

Wanaume wenye magonjwa ya moyo na kisukari huwa na tatizo kubwa la upungufu wa nguvu za kiume.Parachichi pia limeonekana kuwa na faida nyingi katika kuboresha afya ya macho, viungo vya mwili na nyinginezo nyingi.

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA FANGASI UKENI.

Fangasi ukeni ni muwasho sehemu ya ndani ya uke ambao unaweza kuambatana pia na kuvimba kwa uke. Leo sitaongelea sana juu ya nini kinasababisha hizi fangasi sehemu ya uke bali tutaona dozi kamili ya asili inayoweza kutibu kabisa tatizo hili linalosumbuwa wanawake wengi miaka sasa. Tumia dawa hizi 3 zote kwa pamoja ili kupata matokeo mazuri na usiache kuleta mrejesho hapa namna unavyoendelea: 1. LEMONADE Lemonade inaandaliwa kwa kutumia limau, maji, asali na mdalasini ya unga kidogo, nayo inaandaliwa hivi: *Chukua asali mbichi nusu Lita *Chukua limau kubwa 12 au zaidi, zikate katikati kila moja. Zikamuwe moja baada ya nyingine kupata maji maji ya limau mpaka umepata ujazo wa nusu lita. *Kwenye sufuria nyingine kubwa changanya mdalasini ya unga vijiko vikubwa 10 na maji lita 2 na nusu na uchemshe kama chai kisha ipua na uchuje na usubiri ipowe iwe ya uvuguvugu kidogo. *Sasa changanya pamoja asali nusu lita, juisi au maji maji ya limau nusu lita, maji ya uvuguvugu ya m...

TIBA YA MTU ALIEINGIWA NA JINNI SUGU.

kabla sijatoa tiba yake, ni lazima ujue unatibu nini na kwanini ni jinni. Maana zipo dalili mbalimbali zinazoonyesha mgonjwa amehusudiwa na jini na ni jini aina gani aliemuingilia muhusika. Zifuatazo ni aina na utaratibu wa kumtibu jini sugu. Dawa za kula. Habbatsaudai Habbatsufa Bakahadi Manimani Uzile Habbat rehani Karkam Halilinji Alhamza Kamun aswad Zamda Khardal Daarfilfil Filfil aswad Haltit Zaatar Harmal Sufa nyeupe Manimani Shomari Udinadi Ulinjani Sakabanji Kamun abyadh Uwatu Giligilani Karafuu Tangawizi Mdalasini Maua waridi Hakikisha dawa hizi umezitwanga na kuwa laini kisha utachukua kijiko kimoja cha kila dawa na kuchanganya kwenye asali safi ya nyuki lita moja na uisomee ruqya na mgonjwa awe anakunywa vijiko viwili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 30. NB Hakikisha wakati mgonjwa anatumia dawa za kula ambatanishe na za kujifukiza pamoja na za kujipaka. DAWA ZA KUFUKIZA kiribiti upele Sandarusi Haltit Karafuu maiti Mruturutu ...

KICHOMI

  Kichomi   ni moja ya dalili za ugonjwa moyo. Kupatwa kichomi mara moja moja si vibaya. Ukipatwa muda mrefu au kila wakati ; basi, chunguza zaidi. Kichomi husababishwa au kinaweza kuwa. Dalili ya matatizo ya tumbo lenye asidi (acid) kuzidi Dalili za ugonjwa wa moyo uitwao Ischemic Jambo la kuangalia ni je? Unashikwa kichomi ukiwa unatembea? Umeinama au umelala Ukishakula chakula Kama unapatwa kichomi wakati ukitembea au ukishafanya mazoezi makali ina maana kuna tatizo la damu kuingia sawasawa au kuzunguka (circulation) katika moyo. Kama unapatwa kichomi baada ya kula ina maana kuna tatizo katika chakula unachokula. Je mlo wako una acid(uchachu) sana? Je, unakula vyakula vyenye pilipili na binzari(spices) kwa wingi sana? Kama una kula sana vyakula vyenye asidi ina maana tumbo lako halimeng’enyui sawasawa linachoka. Kawaida binadamu unabidi kubadili badili ulaji. Usirudie vitu fulani fulani kila siku. Mathalan usiweke pilipili katika kila mlo. Tatizo ji...