Skip to main content

Posts

Showing posts from October 4, 2017

MAMBO YAKUFANYA ILI MIMBA IWE SALAMA

Kulingana na Hazina ya Umoja wa Mataifa ya Idadi ya Watu,zaidi ya wanawake nusu milioni hufa kila mwaka kutokana na matatizo yanayohusiana na mimba. Isitoshe,Shirika la Umoja wa Mataifa la Hazina ya Watoto linasema kwamba kila mwaka zaidi ya wanawake milioni 60 huugua vibaya wakiwa wajawazito hivi kwamba karibu thuluthi moja kati yao hupata majeraha au maambukizo yanayodumu muda mrefu.     Katika nchi zinazoendelea, wanawake wengi hupata mimba moja baada ya nyingine,hujifungua, na kujiachilia, jambo ambalo huwafanya wawe wachovu na wagonjwa. mimba inaweza kuleta madhara hata kuhatarisha uhai.       JE, MWANAMKE ANAWEZA KUFANYA NINI ILI MIMBA YAKE IWE SALAMA ZAIDI ?   Utunzaji wa Kiafya Kabla ya Kuwa  Mjamzito. 1.Kupanga.  Huenda waume na wake wakahitaji kuzungumza kuhusu idadi ya watoto ambao watapata. Katika nchi zinazoendelea,ni kawaida kuwaona wanawake wenye watoto wanaonyonya wakiwa wajawazito. K...