Skip to main content

UGONJWA WA STROKE ( KIHARUSI )

UGONJWA WA STROKE(KIHARUSI)
Fahamu aina za kiharusi(strocke).


Kiharusi au kwa Kiingereza Stroke ni kitendo cha baadhi ya viungo vya mwili kuwa na ganzi au kutojiweza kufanya kazi zake za kawaida.


Kuna aina mbili za kiharusi,


lakini kabla ya kuchambua hayo tuangalie,ni nini kinasababisha mtu
kukumbwa na ugonjwa huu ?.


Mtu anaweza kupata dalili za ugonjwa huu wa kiharusi na baada ya dakika chake zikaisha.


Kiharusi kinampata binadamu baada ya eneo la ubongo kukosa damu kwa saa 24 ama zaidi au kunapotokea kizuizi cha damu au mishipa ya damu kushindwa kusafirisha damu au mshipa huo
unapopasuka.


Kiharusi kimegawanyika katika aina kuu mbili kulingana na jinsi kinavyotokea.


kwanza ni:

1.Kiharusi cha kukosa hewa kwenye ubongo kitaalamu huitwa Ischemic stroke.

(Ischemic ni neno la Kigiriki lenye maana ya kuzuia damu).


Aina hii ya kiharusi hutokea iwapo usambazaji wa damu katika sehemu ya ubongo hupungua na kusababisha tishu za ubongo za eneo lililoathirika kushindwa kufanya kazi zake vizuri.


Hiki hutokea baada ya mshipa wa ateri kuziba kutokana na kuganda kwa damu,hali ambayo inasababisha damu isisafiri vyema na kuelekea kwenye ubongo.


Hali hiyo pia hufanya damu iliyoganda kuziba mishipa midogo ndani ya ubongo kitaalamu huitwa Cerebral thrombosis au kipande cha damu kumeguka na kwenda kuziba mshipa wa damu kwenye ubongo kitaalamu huitwa Cerebral embolism.


Lakini tatizo hili linaweza kutokea pale damu inapoganda sehemu nyingine ya mwili na kusafiri hadi kwenye mishipa ya ateri,hivyo kusababisha damu kwenda kwenye ubongo kukwama.


Hata hivyo,tatizo hili linaweza
kusababisha kitu kinachoitwa Lacunar stroke,yaani vimirija vidogovidogo sana vya damu vilivyopo ndani ya ubongo,vinaziba.


Hapo sasa binadamu huwa anakumbwa na kiharusi kinachojulikana kitaalamu Lacunar stroke japokuwa mara nyingi hii haiwaletei sana shida wagonjwa.


KIHARUSI CHA HAEMORRHAGE.

Baada ya kufafanua kiharusi kinachoitwa ischaemia ambacho ndani yake tukaelezea pia kile kinachoitwa Lacunar stroke,sasa tuelezee aina ya kiharusi kiitwacho Haemorrhage.


Aina hii ya kiharusi,mrija wa damu karibu ama kwenye ubongo hupata mpasuko hivyo kusababisha damu kuvuja na kitendo hicho ndicho kitaalamu huitwa Haemorrhage.


Kinachotokea ni kwamba damu inayovuja hukandamiza ubongo na kuuharibu,ubongo ni moja ya kiungo laini sana mwilini.Katika hali ya kitaalamu inayoitwa Intra cerebral haemorrhage,uvujaji wa damu hufanyika ndani ya ubongo wenyewe.


Mara nyingi aina hii ya kiharusi hutanguliwa na dalili za kichwa kuuma,au kuwepo kwa historia ya ajali ya kichwa.



Lakini kuna hali pia inayoitwa Subarachnoid haemorrhage ambapo mpasuko wa mshipa wa damu hufanyika karibu na eneo linalozunguka ubongo linaloitwa Subarachnoid.



Wakati fulani,mishipa ya damu huzungukwa na aina fulani za mafuta yasiyofaa mwilini,hali inayoitwa kitaalamu kama Atherosclerotic plaque.


Hali hii husababisha kuganda kwa damu katika mishipa (thrombosis) hiyo.

DALILI ZA STROKES AU KIHARUSI
- kuchanganyikiwa,mtu kupata shida ya kuongea na kuelewa anachoambiwa.
- Maumivu ya kichwa pamoja na kupoteza fahamu kwa vipindi na kutapika
- Ganzi usoni,mkono na mguu na hasa ikiwa ni stroke ya upande mmoja wa mwili
- shida ya kuona
- Shida ya kutembea
Kizunguzungu na kukosa mpangilio wa matendo ya mwili

BAADHI YA ATHARI
- maumivu ya mikono na miguu baada ya viungo hvyo kufanya kazi au kutokea mabadiliko ya hali ya hewa
- Msongo wa mawazo
- Kupooza au udhaifu wa upande1
- Kupata shida ktk kuonyesha hisia za mwili
- Kushindwa kumudu matumizi ya kibofu cha mkojo au viungo vya njia ya haja kubwa

JINSI YA KUZUIA STROKE
- Usitumie dawa za kulevya
- Kula chakula chenye mboga na matunda kwa wingi na chenye cholestrol kidogo.
- Fanya mazoez kila siku
- Hakikisha unadhibiti kiwango cha sukari mwilini
- Jitahidi kupunguza uzito
Acha pombe na sigara

tunazo dawa kamili za kuchua, kunywa za maradhi haya.
+254732917064

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA FANGASI UKENI.

Fangasi ukeni ni muwasho sehemu ya ndani ya uke ambao unaweza kuambatana pia na kuvimba kwa uke. Leo sitaongelea sana juu ya nini kinasababisha hizi fangasi sehemu ya uke bali tutaona dozi kamili ya asili inayoweza kutibu kabisa tatizo hili linalosumbuwa wanawake wengi miaka sasa. Tumia dawa hizi 3 zote kwa pamoja ili kupata matokeo mazuri na usiache kuleta mrejesho hapa namna unavyoendelea: 1. LEMONADE Lemonade inaandaliwa kwa kutumia limau, maji, asali na mdalasini ya unga kidogo, nayo inaandaliwa hivi: *Chukua asali mbichi nusu Lita *Chukua limau kubwa 12 au zaidi, zikate katikati kila moja. Zikamuwe moja baada ya nyingine kupata maji maji ya limau mpaka umepata ujazo wa nusu lita. *Kwenye sufuria nyingine kubwa changanya mdalasini ya unga vijiko vikubwa 10 na maji lita 2 na nusu na uchemshe kama chai kisha ipua na uchuje na usubiri ipowe iwe ya uvuguvugu kidogo. *Sasa changanya pamoja asali nusu lita, juisi au maji maji ya limau nusu lita, maji ya uvuguvugu ya m...

TIBA YA MTU ALIEINGIWA NA JINNI SUGU.

kabla sijatoa tiba yake, ni lazima ujue unatibu nini na kwanini ni jinni. Maana zipo dalili mbalimbali zinazoonyesha mgonjwa amehusudiwa na jini na ni jini aina gani aliemuingilia muhusika. Zifuatazo ni aina na utaratibu wa kumtibu jini sugu. Dawa za kula. Habbatsaudai Habbatsufa Bakahadi Manimani Uzile Habbat rehani Karkam Halilinji Alhamza Kamun aswad Zamda Khardal Daarfilfil Filfil aswad Haltit Zaatar Harmal Sufa nyeupe Manimani Shomari Udinadi Ulinjani Sakabanji Kamun abyadh Uwatu Giligilani Karafuu Tangawizi Mdalasini Maua waridi Hakikisha dawa hizi umezitwanga na kuwa laini kisha utachukua kijiko kimoja cha kila dawa na kuchanganya kwenye asali safi ya nyuki lita moja na uisomee ruqya na mgonjwa awe anakunywa vijiko viwili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 30. NB Hakikisha wakati mgonjwa anatumia dawa za kula ambatanishe na za kujifukiza pamoja na za kujipaka. DAWA ZA KUFUKIZA kiribiti upele Sandarusi Haltit Karafuu maiti Mruturutu ...

KICHOMI

  Kichomi   ni moja ya dalili za ugonjwa moyo. Kupatwa kichomi mara moja moja si vibaya. Ukipatwa muda mrefu au kila wakati ; basi, chunguza zaidi. Kichomi husababishwa au kinaweza kuwa. Dalili ya matatizo ya tumbo lenye asidi (acid) kuzidi Dalili za ugonjwa wa moyo uitwao Ischemic Jambo la kuangalia ni je? Unashikwa kichomi ukiwa unatembea? Umeinama au umelala Ukishakula chakula Kama unapatwa kichomi wakati ukitembea au ukishafanya mazoezi makali ina maana kuna tatizo la damu kuingia sawasawa au kuzunguka (circulation) katika moyo. Kama unapatwa kichomi baada ya kula ina maana kuna tatizo katika chakula unachokula. Je mlo wako una acid(uchachu) sana? Je, unakula vyakula vyenye pilipili na binzari(spices) kwa wingi sana? Kama una kula sana vyakula vyenye asidi ina maana tumbo lako halimeng’enyui sawasawa linachoka. Kawaida binadamu unabidi kubadili badili ulaji. Usirudie vitu fulani fulani kila siku. Mathalan usiweke pilipili katika kila mlo. Tatizo ji...