Skip to main content

Posts

MALARIA

chukua karikariyat kiasi cha gram mia moja, na uchemshe katika maji lita moja hakikisha umeshamsha mpaka imepungua kidogo. Baada ya hapo utachuja na kuifadhi katika sehemu salama. Matumizi Nusu kikombe kutwa mara tatu kwa mda wa siku7. In shaa llah tatizo litaisha.

BAWASILI

Hiki ni kinyama kinachotoka ndani ama nje ya tupu kubwa. Kinapotoka nje huitwa bawasili ya nje na kikitoka ndani nayo itakuwa kinyume chake. Zifuatazo ni baadhi ya tiba za bawasili. Bawasili ya nje Chukua mafuta ya mbono na upake sehemu ilipotoka na uingize ndani. Baada ya kuingiza ndani utachukua dawa zifuatazo na ujifukize . - haltit - kiribiti upele - shubiri nyeusi - kamun aswad - kuzbara - mvuje - majani ya toto la yaliyoanguka yenyewe na uyakate vipande vidogovidogo. Na mgonjwa atachanya zote na kujifukiza sehemu ya haja kubwa mara tatu kwa siku. Na kama itakuwa ni ya ndani ama ya nje mgonjwa anaweza chukua dawa inayoitwa MAKALARZAK na kuchemsha kisha anywe nusu kikombe kutwa mara tatu mpaka atakapo pata nufuu.

KUCHELEWA KUFIKA KILELENI KATIKA TENDO LA NDOA.

paka mafuta meupe ya misk katika dhakari yako saa moja kabla hujaingia katika tendo la ndoa. Hakika ukifanya hivyo utakaa sana katika shughuli hiyo bila kufika kileleni haraka.

UTOSI KUINGIA NDANI KWA MTOTO MCHANGA.

chukua manjano mbichi iponde iwe laini sana, kisha chukua pamba na uiweke ile dawa, kisha muekee mtoto mchanga aliena tatizo hilo utosini. In shaa allah utosi utarudi sawa. Utafanya hivyo kwa siku mara moja mpaka tatizo litakapokwisha.

CHANGO LA KINA MAMA

Kwa mwanamke anaesumbuliwa na tatizo kama hili achukue sanamaki ya unga na karikariyat hakikisha ni ya unga, changanya zote kwa ujazo sawa. Kisha utachota vijiko vitano vya mchanganyiko huo na kuweka katika maji lita moja na nusu na uchemshe mpaka yabaki lita moja. Na mgonjwa anywe nusu kikombe kutwa mara mbili kwa mda wa siku 14. NB:- dawa inatibu mpaka ngiri kwa jinsia zote ( mke na mume ).

KUTAPIKA DAMU

hii mara nyingi husababishwa husababishwa na vidonda vya tumbo au majeraha katika sehemu za ndani ya mwili. Tiba Chukua kuzbara na uiroweke katika siki kali kwa mda wa masaa 24 na baada ya kuroweka atie sukari na anywe kikombe cha kahawa mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 3.in shaa allah kutafunga kutapika. NB:- hakikisha kabla hujatumia dawa yeyote upate  vipimo.

NGUVU ZA KIUME ( MTU ANAENDA SAFARI MOJA KATIKA TENDO LA NDOA )

chukua unga wa mzizi wa mjafaar na unga wa mbegu za tikiti maji changanya pamoja sawa kwa sawa na iwe unatia katika maji ya moto glass moja kwa kijiko kimoja. Utafanya zoezi hili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 21. In shaa allah utakuwa na nguvu za ajabu.