Melanoma ni saratani hatari sana kwa maisha ya mwanadamu. Saratani hii huwapata watu wachache lakini inapotokea mtu akapata saratani hii basi maisha yake huwa hatarini. Saratani hii si rahisi kugundulika ikilinganishwa na saratani nyingine za ngozi. Siyo tu kwamba saratani hii ni ngumu kidogo kutambulika bali pia husambaa haraka zaidi kuliko saratani nyingine za ngozi. Melanoma huweza kusambaa na kushambulia viungo vingine zaidi ya ngozi kama mifupa na ubongo. Inapofikia hatua hii saratani hii huwa ngumu sana kutibika.
Ni nani wanaoweza kupata kansa ya ngozi? Mbali na watu ambao wamewahi kupigwa na jua kwa muda mrefu sana, au wale wanaojianika juani kwa vipindi virefu, wale walio na ngozi nyeupe, nywele na macho ya rangi hafifu, wenye mabaka na madoadoa, na wale ambao mtu fulani katika familia yao amekuwa na ugonjwa huo, wanaweza kuupata. Watu weupe hupatwa na kansa ya ngozi zaidi kuliko watu weusi. Lakini je, hii inamaanisha kwamba kadiri ngozi yako inavyounguzwa na jua na kuwa nyeusi ndivyo inavyokuwa vigumu kupatwa na kansa ya ngozi? Sivyo, kwa sababu ingawa ngozi hujigeuza rangi na kuwa nyeusi ili kujikinga na mnururisho wa miale ya jua, lakini inapofanya hivyo huathirika, na inapoathirika mara nyingi huwa kuna uwezekano mkubwa wa kupata kansa ya ngozi.
Dalili za Melanoma
Kuna dalili nyingi za saratani hii na ni vyema kila mtu azifahamu. Dalili ya kwanza kabisa ambayo inabidi kila mtu aifahamu ni kubadilika kwa ukubwa, rangi au ule muundo wa ngozi ambayo umekuwa nayo kwa muda mrefu au umezaliwa nayo. Alama hii ni ile ambayo ina rangi nyeusi zaidi ikilinganishwa na maeneo mengine ya ngozi. Mabadiliko haya si lazima yawe yanatokea haraka haraka yanaweza kuwa yanatokea taratibu katika kipindi cha miezi lakini cha muhimu zaidi ni kuonekana mabadiliko kwenye alama hiyo ya ngozi. Mabadiliko mengine ni kama yafuatayo, alama hiyo inayojitokeza kwenye ngozi inaweza kuwa inavimba, kingo zake kupoteza mzingo wake wa kawaida na alama kua zaidi kwa mfano kutoka mzingo wa milimita 4 na kuzidi milimeta 6. Dalili nyingine ni alama kuanza kuwasha na kama mgonjwa atachelewa kugundua tatizo basi zitajitokeza alama nyingine kwenye ngozi ambayo itapasuka na kuwa kidonda. Alama hiyo baadaye inaweza kutoa damu na kuwa na maumivu.
Kama matibabu hayatafanyika basi saratani hii ya ngozi husambaa na dalili zifuatazo kuonekana:- Tezi za mwili za kwenye makwapa na kwenye nyonga huvimba, mgonjwa kutokwa na uvimbe kwenye ngozi, kupoteza uzito kwa kasi bila kujua sababu, kupata kikohozi kisichoisha, kupoteza fahamu au kupata kifafa, na pia kuumwa na kichwa.
Kwa tiba na maradhi mbalimbali wasiliana nasi.
Comments
Post a Comment