Skip to main content

SARATANI YA NGOZI (MELANOMA )


Melanoma ni saratani hatari sana kwa maisha ya mwanadamu. Saratani hii huwapata watu wachache lakini inapotokea mtu akapata saratani hii basi maisha yake huwa hatarini. Saratani hii si rahisi kugundulika ikilinganishwa na saratani nyingine za ngozi. Siyo tu kwamba saratani hii ni ngumu kidogo kutambulika bali pia husambaa haraka zaidi kuliko saratani nyingine za ngozi. Melanoma huweza kusambaa na kushambulia viungo vingine zaidi ya ngozi kama mifupa na ubongo. Inapofikia hatua hii saratani hii huwa ngumu sana kutibika.
Ni nani wanaoweza kupata kansa ya ngozi? Mbali na watu ambao wamewahi kupigwa na jua kwa muda mrefu sana, au wale wanaojianika juani kwa vipindi virefu, wale walio na ngozi nyeupe, nywele na macho ya rangi hafifu, wenye mabaka na madoadoa, na wale ambao mtu fulani katika familia yao amekuwa na ugonjwa huo, wanaweza kuupata. Watu weupe hupatwa na kansa ya ngozi zaidi kuliko watu weusi. Lakini je, hii inamaanisha kwamba kadiri ngozi yako inavyounguzwa na jua na kuwa nyeusi ndivyo inavyokuwa vigumu kupatwa na kansa ya ngozi? Sivyo, kwa sababu ingawa ngozi hujigeuza rangi na kuwa nyeusi ili kujikinga na mnururisho wa miale ya jua, lakini inapofanya hivyo huathirika, na inapoathirika mara nyingi huwa kuna uwezekano mkubwa wa kupata kansa ya ngozi.


Dalili za Melanoma
Kuna dalili nyingi za saratani hii na ni vyema kila mtu azifahamu. Dalili ya kwanza kabisa ambayo inabidi kila mtu aifahamu ni kubadilika kwa ukubwa, rangi au ule muundo wa ngozi ambayo umekuwa nayo kwa muda mrefu au umezaliwa nayo. Alama hii ni ile ambayo ina rangi nyeusi zaidi ikilinganishwa na maeneo mengine ya ngozi. Mabadiliko haya si lazima yawe yanatokea haraka haraka yanaweza kuwa yanatokea taratibu katika kipindi cha miezi lakini cha muhimu zaidi ni kuonekana mabadiliko kwenye alama hiyo ya ngozi. Mabadiliko mengine ni kama yafuatayo, alama hiyo inayojitokeza kwenye ngozi inaweza kuwa inavimba, kingo zake kupoteza mzingo wake wa kawaida na alama kua zaidi kwa mfano kutoka mzingo wa milimita 4 na kuzidi milimeta 6. Dalili nyingine ni alama kuanza kuwasha na kama mgonjwa atachelewa kugundua tatizo basi zitajitokeza alama nyingine kwenye ngozi ambayo itapasuka na kuwa kidonda. Alama hiyo baadaye inaweza kutoa damu na kuwa na maumivu.
Kama matibabu hayatafanyika basi saratani hii ya ngozi husambaa na dalili zifuatazo kuonekana:- Tezi za mwili za kwenye makwapa na kwenye nyonga huvimba, mgonjwa kutokwa na uvimbe kwenye ngozi, kupoteza uzito kwa kasi bila kujua sababu, kupata kikohozi kisichoisha, kupoteza fahamu au kupata kifafa, na pia kuumwa na kichwa.
Kwa tiba na maradhi mbalimbali wasiliana nasi.

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA FANGASI UKENI.

Fangasi ukeni ni muwasho sehemu ya ndani ya uke ambao unaweza kuambatana pia na kuvimba kwa uke. Leo sitaongelea sana juu ya nini kinasababisha hizi fangasi sehemu ya uke bali tutaona dozi kamili ya asili inayoweza kutibu kabisa tatizo hili linalosumbuwa wanawake wengi miaka sasa. Tumia dawa hizi 3 zote kwa pamoja ili kupata matokeo mazuri na usiache kuleta mrejesho hapa namna unavyoendelea: 1. LEMONADE Lemonade inaandaliwa kwa kutumia limau, maji, asali na mdalasini ya unga kidogo, nayo inaandaliwa hivi: *Chukua asali mbichi nusu Lita *Chukua limau kubwa 12 au zaidi, zikate katikati kila moja. Zikamuwe moja baada ya nyingine kupata maji maji ya limau mpaka umepata ujazo wa nusu lita. *Kwenye sufuria nyingine kubwa changanya mdalasini ya unga vijiko vikubwa 10 na maji lita 2 na nusu na uchemshe kama chai kisha ipua na uchuje na usubiri ipowe iwe ya uvuguvugu kidogo. *Sasa changanya pamoja asali nusu lita, juisi au maji maji ya limau nusu lita, maji ya uvuguvugu ya m...

TIBA YA MTU ALIEINGIWA NA JINNI SUGU.

kabla sijatoa tiba yake, ni lazima ujue unatibu nini na kwanini ni jinni. Maana zipo dalili mbalimbali zinazoonyesha mgonjwa amehusudiwa na jini na ni jini aina gani aliemuingilia muhusika. Zifuatazo ni aina na utaratibu wa kumtibu jini sugu. Dawa za kula. Habbatsaudai Habbatsufa Bakahadi Manimani Uzile Habbat rehani Karkam Halilinji Alhamza Kamun aswad Zamda Khardal Daarfilfil Filfil aswad Haltit Zaatar Harmal Sufa nyeupe Manimani Shomari Udinadi Ulinjani Sakabanji Kamun abyadh Uwatu Giligilani Karafuu Tangawizi Mdalasini Maua waridi Hakikisha dawa hizi umezitwanga na kuwa laini kisha utachukua kijiko kimoja cha kila dawa na kuchanganya kwenye asali safi ya nyuki lita moja na uisomee ruqya na mgonjwa awe anakunywa vijiko viwili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 30. NB Hakikisha wakati mgonjwa anatumia dawa za kula ambatanishe na za kujifukiza pamoja na za kujipaka. DAWA ZA KUFUKIZA kiribiti upele Sandarusi Haltit Karafuu maiti Mruturutu ...

KICHOMI

  Kichomi   ni moja ya dalili za ugonjwa moyo. Kupatwa kichomi mara moja moja si vibaya. Ukipatwa muda mrefu au kila wakati ; basi, chunguza zaidi. Kichomi husababishwa au kinaweza kuwa. Dalili ya matatizo ya tumbo lenye asidi (acid) kuzidi Dalili za ugonjwa wa moyo uitwao Ischemic Jambo la kuangalia ni je? Unashikwa kichomi ukiwa unatembea? Umeinama au umelala Ukishakula chakula Kama unapatwa kichomi wakati ukitembea au ukishafanya mazoezi makali ina maana kuna tatizo la damu kuingia sawasawa au kuzunguka (circulation) katika moyo. Kama unapatwa kichomi baada ya kula ina maana kuna tatizo katika chakula unachokula. Je mlo wako una acid(uchachu) sana? Je, unakula vyakula vyenye pilipili na binzari(spices) kwa wingi sana? Kama una kula sana vyakula vyenye asidi ina maana tumbo lako halimeng’enyui sawasawa linachoka. Kawaida binadamu unabidi kubadili badili ulaji. Usirudie vitu fulani fulani kila siku. Mathalan usiweke pilipili katika kila mlo. Tatizo ji...