Skip to main content

DEGEDEGE

Degedege Ni Nini ?

Ni hali ya ghafla ya kutingishika kwa mwili mzima au miguu na mikono,ambayo husababishwa na kukakamaa kwa misuli ya mwili.


Hali hii uhusishwa na magonjwa ya ubongo kama kifafa,vichocheo vya kwenye damu kama upungufu wa sukari(hypoglycemia), upungufu wa oxygen(hypoxia),kushuka kwa shinikizo la damu(hypotension) na maambukizi na homa ya degedege.


Homa ni Nini ?.


Ni hali ya kawaida ya mwili kushindwa kujikinga na maambukizi.


Na kwa watoto hutokea pale joto la mwili linapokuwa zaidi ya nyuzi 38 za sentigredi.


Homa ya Degedege Ni Nini ?.

Ni degedege linalotokea kwa watoto ghafla likiambatana na homa kali iliyotokana na kuongezeka haraka kwa joto la mwili.

Ugonjwa huu utokea kwa wastani wa asilimia nne (4%) ya watoto walio kati ya umri wa miezi sita na miaka mitano.


Watoto wengi ambao hupatwa na ugonjwa huu huwa haiwapelekei baadae kuwa na matatizo ya kudumu kama kupata ugonjwa wa kifafa,niasilimia tatu (3%) tu ambao wanaweza baadae kupata ugonjwa wa kifafa.


Mmoja kati ya watoto watatu anbao wamewahi kuwa na homa ya degedege wanaweza wakapatwa tena na tatizo hili.


baadhi ya watoto wanaweza wasipatwe kabisa na tatizo hili au wakapatwa mara moja tu kwa maisha yao yote.


Lakini hauna jinsi ya kutabiri ni mtoto yupi ambaye anaweza kupatwa na shambulio hili.


Homa ya Degedege Hutokea kwa Watoto Gani ?.

Watoto wanaweza kurithi tabia hii ya kuumwa homa ya degedege kutoka kwa wazazi wao.


Kama mama au baba aliwahi kuumwa ugonjwa huu basi mtoto ana asilimia 10-20 zaidi ya kuumwa ugonjwa huu hukilinganisha na yule ambaye wazazi wake hawakuwai kuumwa ugonjwa huu.


Homa isababishwayo na maabukizi yoyote yale kama virus,bakteria na parasite.


Dalili za Homa ya Degedege ni Zipi ?.


Shambulio la ugonjwa huu likijitokeza mtoto uanza na kupotewa na fahamu na muda mfupi baadae mwili,miguu na mikono uanza kukakamaa na kurudisha kichwa nyuma,baada ya hayo miguu na mikono uanza kujitikisa.


Kushindwa kupumua na kutokwa na mapovu mdomoni.

Macho kugeukia nyuma na kuonekana kwa sehemu nyeupe ya jicho.

Shambulio huisha baada ya muda mfupi mara nyingi chini ya dakika tano


Baada ya shambulio mtoto hupitiwa na usingizi mzito kama takribani dakika 30 hadi saa nzima.


Akizinduka anaweza kushindwa hata kukutambua na akawa atamani kitu chochote kwa muda huo.


Nini cha Kufanya Mtoto anapopatwa na Shambulio.

Tulia na usichanganyikiwe.

Ondoa vitu vya hatari karibu na mtoto na muweke sehemu ya usalama kama sakafuni.

Usijaribu kuweka kitu chochote mdomoni kwa mtoto hata vidole vyako.

Angalia muda wa shambulio kuanza hadi litakapo isha ili umueleze daktari.

Baada ya shambulio kuisha mlaze mtoto kwa upande na usimuamshe muache apumzike.

Shambulio la homa ya degedege sio kifafa na mtoto hapati maumivu yoyote wakati wa shambulio kwa hiyo usimpe dawa yoyote ile.

Kwa tiba kamili wasiliana nasi.

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA FANGASI UKENI.

Fangasi ukeni ni muwasho sehemu ya ndani ya uke ambao unaweza kuambatana pia na kuvimba kwa uke. Leo sitaongelea sana juu ya nini kinasababisha hizi fangasi sehemu ya uke bali tutaona dozi kamili ya asili inayoweza kutibu kabisa tatizo hili linalosumbuwa wanawake wengi miaka sasa. Tumia dawa hizi 3 zote kwa pamoja ili kupata matokeo mazuri na usiache kuleta mrejesho hapa namna unavyoendelea: 1. LEMONADE Lemonade inaandaliwa kwa kutumia limau, maji, asali na mdalasini ya unga kidogo, nayo inaandaliwa hivi: *Chukua asali mbichi nusu Lita *Chukua limau kubwa 12 au zaidi, zikate katikati kila moja. Zikamuwe moja baada ya nyingine kupata maji maji ya limau mpaka umepata ujazo wa nusu lita. *Kwenye sufuria nyingine kubwa changanya mdalasini ya unga vijiko vikubwa 10 na maji lita 2 na nusu na uchemshe kama chai kisha ipua na uchuje na usubiri ipowe iwe ya uvuguvugu kidogo. *Sasa changanya pamoja asali nusu lita, juisi au maji maji ya limau nusu lita, maji ya uvuguvugu ya m...

TIBA YA MTU ALIEINGIWA NA JINNI SUGU.

kabla sijatoa tiba yake, ni lazima ujue unatibu nini na kwanini ni jinni. Maana zipo dalili mbalimbali zinazoonyesha mgonjwa amehusudiwa na jini na ni jini aina gani aliemuingilia muhusika. Zifuatazo ni aina na utaratibu wa kumtibu jini sugu. Dawa za kula. Habbatsaudai Habbatsufa Bakahadi Manimani Uzile Habbat rehani Karkam Halilinji Alhamza Kamun aswad Zamda Khardal Daarfilfil Filfil aswad Haltit Zaatar Harmal Sufa nyeupe Manimani Shomari Udinadi Ulinjani Sakabanji Kamun abyadh Uwatu Giligilani Karafuu Tangawizi Mdalasini Maua waridi Hakikisha dawa hizi umezitwanga na kuwa laini kisha utachukua kijiko kimoja cha kila dawa na kuchanganya kwenye asali safi ya nyuki lita moja na uisomee ruqya na mgonjwa awe anakunywa vijiko viwili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 30. NB Hakikisha wakati mgonjwa anatumia dawa za kula ambatanishe na za kujifukiza pamoja na za kujipaka. DAWA ZA KUFUKIZA kiribiti upele Sandarusi Haltit Karafuu maiti Mruturutu ...

KICHOMI

  Kichomi   ni moja ya dalili za ugonjwa moyo. Kupatwa kichomi mara moja moja si vibaya. Ukipatwa muda mrefu au kila wakati ; basi, chunguza zaidi. Kichomi husababishwa au kinaweza kuwa. Dalili ya matatizo ya tumbo lenye asidi (acid) kuzidi Dalili za ugonjwa wa moyo uitwao Ischemic Jambo la kuangalia ni je? Unashikwa kichomi ukiwa unatembea? Umeinama au umelala Ukishakula chakula Kama unapatwa kichomi wakati ukitembea au ukishafanya mazoezi makali ina maana kuna tatizo la damu kuingia sawasawa au kuzunguka (circulation) katika moyo. Kama unapatwa kichomi baada ya kula ina maana kuna tatizo katika chakula unachokula. Je mlo wako una acid(uchachu) sana? Je, unakula vyakula vyenye pilipili na binzari(spices) kwa wingi sana? Kama una kula sana vyakula vyenye asidi ina maana tumbo lako halimeng’enyui sawasawa linachoka. Kawaida binadamu unabidi kubadili badili ulaji. Usirudie vitu fulani fulani kila siku. Mathalan usiweke pilipili katika kila mlo. Tatizo ji...