Skip to main content

UCHI KULEGEA

Jee, wewe ni mmojawapo wa wale wanawake wanaohisi kuwa na tatizo la uchi kulegea? Haupo peke yako, wanawake wengi wanatatizwa na jambo hili, wanaweza kuwa wameambiwa jambo hili na wapenzi wao au wao wenyewe walijaribu kujipima kwa kujiingiza vidole kwenye sehemu hizo za siri. Katika makala hii natumia neno uchi, ambalo si neno sahihi sana, nikimaanisha sehemu ya nyeti za mwanamke ambayo hutumika wakati wa kufanya mapenzi, kupitisha damu chafu wakati wa siku za hedhi na kupitisha mtoto wakati anapozaliwa. Neno sahihi ni Kuma. Nalitumia neno hilo kukudhi haja ya wengi waliolizoea. Maneno mengine ambayo yamezoeleka kueleza tatizo hilo ni uchi mpana, uchi mkubwa na mengineyo.

Dalili Za Uchi Kulegea

Kabla ya yote tutazame uchi huu ulivyoumbwa. Uchi ni kama kijimfuko kirefu kilichozungukwa na misuli ambacho kwa ndani kimezungukwa na utando laini unaovutika wenye unyevunyevu unaosaidia kupunguza msuguano na wenye uwezo wa kuleta hisia za mapenzi. Kabla mwanamke hajawa tayari kwa mapenzi, kijimfuko hiki huwa kidogo chenye urefu wa inchi 2.75 hadi inchi 3.25 na upana wa robo tatu ya inchi kule ndani kinapoishia. Baada ya kuwa tayari kufanya mapenzi, kijimfuko hiki hunyumbuka hadi kufikia urefu wa inchi 5.25 na kutanuka hadi kufikia upana wa inchi 2.5 ndani kinakoishia.
Takwimu za urefu wa uchi hazina maana sana kwetu kwa somo la leo – ni upana ndio tunaotaka kuuzungumzia. Upana huu unaweza kuongezeka kwa kulegea misuli inayouzunguka uchi au kwa kuumbwa na misuli yenye unene mdogo.
Ifahamike kuwa ni kitu cha kawaida misuli hii kulegea umri wa mwanamke unapozidi miaka 60. Sasa kama ni kweli uchi wako umelegea, utaweza kujigundua kwa kuona dalili zifuatazo:
  •          Kufanya tendo la ndoa hakutakupa starehe sana
  •          Kufanya tendo la ndoa hakutampa starehe sana mpenzi wako
  •         Kama utahisi kwamba hewa inaingia na kutoka kwenye uchi              wako (fanny farting)
  •         Ukiona mkojo unavuja hasa unapocheka, kupiga chafya au                  kukohoa.

 Sababu Za Uchi Kulegea

Kama wewe ni msichana au mwanamke ambaye hujawahi kuzaa hata mara moja, suala la wewe kuwa na uchi mpana ni la kufikirika, uwezekano ni mdogo mno au ni finyu. Kuna dhana iliyoenea kwamba mwanamke anayeshiriki ngono sana atakuwa na uchi uliolegea – Huu ni Upuuzi kabisa! Mwanamke hata akifanya ngono kiasi gani, uchi hauwezi kuwa mpana eti kwa sababu hiyo.
Sababu kubwa ya kuwa na uchi uliolegea kwa mwanamke ni tendo la Uzazi. Mwanamke anapozaa misuli inayozunguka uchi na vitu vyote vinavyoshikilia kuta za uchi huo huathirika na kupungua nguvu kwa kiasi fulani. Hivyo basi, kila unapozaa, ndivyo unavyoiathiri misuli yako zaidi. Mwanamke mwenye watoto wengi sana, uchi wake utakuwa umeathirika zaidi. Namna ulivyozaa pia inaweza kuchangia, kwa mfano kuzaa kwa matatizo (Plonged labours).

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA FANGASI UKENI.

Fangasi ukeni ni muwasho sehemu ya ndani ya uke ambao unaweza kuambatana pia na kuvimba kwa uke. Leo sitaongelea sana juu ya nini kinasababisha hizi fangasi sehemu ya uke bali tutaona dozi kamili ya asili inayoweza kutibu kabisa tatizo hili linalosumbuwa wanawake wengi miaka sasa. Tumia dawa hizi 3 zote kwa pamoja ili kupata matokeo mazuri na usiache kuleta mrejesho hapa namna unavyoendelea: 1. LEMONADE Lemonade inaandaliwa kwa kutumia limau, maji, asali na mdalasini ya unga kidogo, nayo inaandaliwa hivi: *Chukua asali mbichi nusu Lita *Chukua limau kubwa 12 au zaidi, zikate katikati kila moja. Zikamuwe moja baada ya nyingine kupata maji maji ya limau mpaka umepata ujazo wa nusu lita. *Kwenye sufuria nyingine kubwa changanya mdalasini ya unga vijiko vikubwa 10 na maji lita 2 na nusu na uchemshe kama chai kisha ipua na uchuje na usubiri ipowe iwe ya uvuguvugu kidogo. *Sasa changanya pamoja asali nusu lita, juisi au maji maji ya limau nusu lita, maji ya uvuguvugu ya m...

TIBA YA MTU ALIEINGIWA NA JINNI SUGU.

kabla sijatoa tiba yake, ni lazima ujue unatibu nini na kwanini ni jinni. Maana zipo dalili mbalimbali zinazoonyesha mgonjwa amehusudiwa na jini na ni jini aina gani aliemuingilia muhusika. Zifuatazo ni aina na utaratibu wa kumtibu jini sugu. Dawa za kula. Habbatsaudai Habbatsufa Bakahadi Manimani Uzile Habbat rehani Karkam Halilinji Alhamza Kamun aswad Zamda Khardal Daarfilfil Filfil aswad Haltit Zaatar Harmal Sufa nyeupe Manimani Shomari Udinadi Ulinjani Sakabanji Kamun abyadh Uwatu Giligilani Karafuu Tangawizi Mdalasini Maua waridi Hakikisha dawa hizi umezitwanga na kuwa laini kisha utachukua kijiko kimoja cha kila dawa na kuchanganya kwenye asali safi ya nyuki lita moja na uisomee ruqya na mgonjwa awe anakunywa vijiko viwili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 30. NB Hakikisha wakati mgonjwa anatumia dawa za kula ambatanishe na za kujifukiza pamoja na za kujipaka. DAWA ZA KUFUKIZA kiribiti upele Sandarusi Haltit Karafuu maiti Mruturutu ...

KICHOMI

  Kichomi   ni moja ya dalili za ugonjwa moyo. Kupatwa kichomi mara moja moja si vibaya. Ukipatwa muda mrefu au kila wakati ; basi, chunguza zaidi. Kichomi husababishwa au kinaweza kuwa. Dalili ya matatizo ya tumbo lenye asidi (acid) kuzidi Dalili za ugonjwa wa moyo uitwao Ischemic Jambo la kuangalia ni je? Unashikwa kichomi ukiwa unatembea? Umeinama au umelala Ukishakula chakula Kama unapatwa kichomi wakati ukitembea au ukishafanya mazoezi makali ina maana kuna tatizo la damu kuingia sawasawa au kuzunguka (circulation) katika moyo. Kama unapatwa kichomi baada ya kula ina maana kuna tatizo katika chakula unachokula. Je mlo wako una acid(uchachu) sana? Je, unakula vyakula vyenye pilipili na binzari(spices) kwa wingi sana? Kama una kula sana vyakula vyenye asidi ina maana tumbo lako halimeng’enyui sawasawa linachoka. Kawaida binadamu unabidi kubadili badili ulaji. Usirudie vitu fulani fulani kila siku. Mathalan usiweke pilipili katika kila mlo. Tatizo ji...