Skip to main content

KICHOMI


     Kichomi ni moja ya dalili za ugonjwa moyo. Kupatwa kichomi mara moja moja si vibaya. Ukipatwa muda mrefu au kila wakati ; basi, chunguza zaidi.
    Kichomi husababishwa au kinaweza kuwa.
    1. Dalili ya matatizo ya tumbo lenye asidi (acid) kuzidi
    2. Dalili za ugonjwa wa moyo uitwao Ischemic
    Jambo la kuangalia ni je?
    1. Unashikwa kichomi ukiwa unatembea?
    2. Umeinama au umelala
    3. Ukishakula chakula

    Kama unapatwa kichomi wakati ukitembea au ukishafanya mazoezi makali ina maana kuna tatizo la damu kuingia sawasawa au kuzunguka (circulation) katika moyo.
    Kama unapatwa kichomi baada ya kula ina maana kuna tatizo katika chakula unachokula. Je mlo wako una acid(uchachu) sana? Je, unakula vyakula vyenye pilipili na binzari(spices) kwa wingi sana? Kama una kula sana vyakula vyenye asidi ina maana tumbo lako halimeng’enyui sawasawa linachoka.
    Kawaida binadamu unabidi kubadili badili ulaji. Usirudie vitu fulani fulani kila siku. Mathalan usiweke pilipili katika kila mlo.
    Tatizo jingine ni ulaji wa chakula chenye chumvi nyingi sana. Chumvi inakorofisha pia mzunguko wa damu mwilini.
    Tiba
    Chukua sanamaki ya unga vijiko 5 na uchemshe kwa maji lita moja na nusu na uchemshe kwa maji lita na nusu uchemshe mpaka ibaki lita moja na unywe yote ikiwa vuguvugu. pia hakikisha umekunywa maji mengi mara kwa mara.

    Kwa maelezo zaidi wasiliana nami.
    +254732917064.

    Comments

    Popular posts from this blog

    TIBA YA MTU ALIEINGIWA NA JINNI SUGU.

    kabla sijatoa tiba yake, ni lazima ujue unatibu nini na kwanini ni jinni. Maana zipo dalili mbalimbali zinazoonyesha mgonjwa amehusudiwa na jini na ni jini aina gani aliemuingilia muhusika. Zifuatazo ni aina na utaratibu wa kumtibu jini sugu. Dawa za kula. Habbatsaudai Habbatsufa Bakahadi Manimani Uzile Habbat rehani Karkam Halilinji Alhamza Kamun aswad Zamda Khardal Daarfilfil Filfil aswad Haltit Zaatar Harmal Sufa nyeupe Manimani Shomari Udinadi Ulinjani Sakabanji Kamun abyadh Uwatu Giligilani Karafuu Tangawizi Mdalasini Maua waridi Hakikisha dawa hizi umezitwanga na kuwa laini kisha utachukua kijiko kimoja cha kila dawa na kuchanganya kwenye asali safi ya nyuki lita moja na uisomee ruqya na mgonjwa awe anakunywa vijiko viwili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 30. NB Hakikisha wakati mgonjwa anatumia dawa za kula ambatanishe na za kujifukiza pamoja na za kujipaka. DAWA ZA KUFUKIZA kiribiti upele Sandarusi Haltit Karafuu maiti Mruturutu ...

    KUONDOSHA MARADHI YA SUBIAN NA KUONDOA WASIWASI

    Kwa mtu mwenye matatizo hayo achukue dawa zifuatazo :- - unga wa ambari nyeusi. - unga wa mvuje. - unga wa kitunguu thaum. - mafuta ya uto. - mafuta original ya zaituni. Maelezo Changanya na iwe unajipaka mwili mzima asubuhi na jioni kwa mda wa siku 21.

    UTOSI KUINGIA NDANI KWA MTOTO MCHANGA.

    chukua manjano mbichi iponde iwe laini sana, kisha chukua pamba na uiweke ile dawa, kisha muekee mtoto mchanga aliena tatizo hilo utosini. In shaa allah utosi utarudi sawa. Utafanya hivyo kwa siku mara moja mpaka tatizo litakapokwisha.