Skip to main content

UGONJWA WA RETINA UNAOSABABISHWA NA KISUKARI



Jicho ni kiungo ambacho binadamu anapaswa kuwa makini kukilinda maana kuwapo kwake kunasaidia viungo kutenda kazi vyema.

idadi ya wagonjwa wengi wakisukari nchini na duniani inazidi kuongezeka. Ugonjwa huu wa macho huwapata watu wenye
kisukari cha muda mrefu.

Kuwapo kwa ugonjwa wa kisukari husababisha kuharibika kwa retina.

Hii ni sehemu ya nyuma ya jicho
ambayo inaundwa kwa utando wa neva ama mishipa ya fahamu.

Mishipa hii ya fahamu ni muhimu sana katika kumuwezesha mtu
kuona. Ndio inayopokea taswira ya vitu na kuipeleka katika ubongo kwa ajili ya tafsiri.

Kuathirika kwa neva hizi ni tatizo la hatari kwa uwezo wa jicho kuona kwani inaweza kusababisha kuwa na uwezo mdogo wa kutambua taswira ya vitu. Hali hii isipotibiwa
mapema, husababisha ulemavu wa kudumu.

Kisukari ni ugonjwa unaoingilia uwezo wa mwili kutumia na kuhifadhi sukari mwilini. Hii husababisha madhara makubwa mwilini. Sukari ndio nishati inayotegemewa na mwili katika kuendesha shughuli mbalimbali.

Kwa kawaida sukari katika mwili inatakiwa iwe katika kipimo cha saba hadi 12 (7-12).

Uwapo wa sukari nyingi katika
mzunguko wa damu husababisha madhara mbalimbali mwilini ikiwamo sehemu ya jicho ya nyuma
iitwayo retina.

Kadri sukari inavyozidi na muda unavyosogea, mfumo wa mzunguko wa damu katika jicho huathirika.

Ugonjwa hutokea pale sehemu ya retina inapokosa lishe kutoka kwenye vishipa vidogo
vinavyoathirika kutokana na wingi wa sukari mwilini.

Hali hii ikiendelea husababisha mishipa kuvujisha damu na maji maji hivyo kuzifanya tishu za retina
kuvimba na kuwapo na taswira yenye ukungu.

Tatizo hili huathiri macho yote
mawili na kadri mtu anavyoendelea kuugua kisukari ndivyo anavyokua
katika hatari ya kuathirika na
ugonjwa huu zaidi.

Dalili za ugonjwa huu Kuona ukungu au vidoadoa katika taswira unayotazama. Inawezekana pia akaona mawimbi wakati wa kutazama kitu, kushindwa kuona vizuri hasa nyakati za usiku, kuona
giza au kidoa katikati ya taswira imayoonekana.

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA FANGASI UKENI.

Fangasi ukeni ni muwasho sehemu ya ndani ya uke ambao unaweza kuambatana pia na kuvimba kwa uke. Leo sitaongelea sana juu ya nini kinasababisha hizi fangasi sehemu ya uke bali tutaona dozi kamili ya asili inayoweza kutibu kabisa tatizo hili linalosumbuwa wanawake wengi miaka sasa. Tumia dawa hizi 3 zote kwa pamoja ili kupata matokeo mazuri na usiache kuleta mrejesho hapa namna unavyoendelea: 1. LEMONADE Lemonade inaandaliwa kwa kutumia limau, maji, asali na mdalasini ya unga kidogo, nayo inaandaliwa hivi: *Chukua asali mbichi nusu Lita *Chukua limau kubwa 12 au zaidi, zikate katikati kila moja. Zikamuwe moja baada ya nyingine kupata maji maji ya limau mpaka umepata ujazo wa nusu lita. *Kwenye sufuria nyingine kubwa changanya mdalasini ya unga vijiko vikubwa 10 na maji lita 2 na nusu na uchemshe kama chai kisha ipua na uchuje na usubiri ipowe iwe ya uvuguvugu kidogo. *Sasa changanya pamoja asali nusu lita, juisi au maji maji ya limau nusu lita, maji ya uvuguvugu ya m...

TIBA YA MTU ALIEINGIWA NA JINNI SUGU.

kabla sijatoa tiba yake, ni lazima ujue unatibu nini na kwanini ni jinni. Maana zipo dalili mbalimbali zinazoonyesha mgonjwa amehusudiwa na jini na ni jini aina gani aliemuingilia muhusika. Zifuatazo ni aina na utaratibu wa kumtibu jini sugu. Dawa za kula. Habbatsaudai Habbatsufa Bakahadi Manimani Uzile Habbat rehani Karkam Halilinji Alhamza Kamun aswad Zamda Khardal Daarfilfil Filfil aswad Haltit Zaatar Harmal Sufa nyeupe Manimani Shomari Udinadi Ulinjani Sakabanji Kamun abyadh Uwatu Giligilani Karafuu Tangawizi Mdalasini Maua waridi Hakikisha dawa hizi umezitwanga na kuwa laini kisha utachukua kijiko kimoja cha kila dawa na kuchanganya kwenye asali safi ya nyuki lita moja na uisomee ruqya na mgonjwa awe anakunywa vijiko viwili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 30. NB Hakikisha wakati mgonjwa anatumia dawa za kula ambatanishe na za kujifukiza pamoja na za kujipaka. DAWA ZA KUFUKIZA kiribiti upele Sandarusi Haltit Karafuu maiti Mruturutu ...

KICHOMI

  Kichomi   ni moja ya dalili za ugonjwa moyo. Kupatwa kichomi mara moja moja si vibaya. Ukipatwa muda mrefu au kila wakati ; basi, chunguza zaidi. Kichomi husababishwa au kinaweza kuwa. Dalili ya matatizo ya tumbo lenye asidi (acid) kuzidi Dalili za ugonjwa wa moyo uitwao Ischemic Jambo la kuangalia ni je? Unashikwa kichomi ukiwa unatembea? Umeinama au umelala Ukishakula chakula Kama unapatwa kichomi wakati ukitembea au ukishafanya mazoezi makali ina maana kuna tatizo la damu kuingia sawasawa au kuzunguka (circulation) katika moyo. Kama unapatwa kichomi baada ya kula ina maana kuna tatizo katika chakula unachokula. Je mlo wako una acid(uchachu) sana? Je, unakula vyakula vyenye pilipili na binzari(spices) kwa wingi sana? Kama una kula sana vyakula vyenye asidi ina maana tumbo lako halimeng’enyui sawasawa linachoka. Kawaida binadamu unabidi kubadili badili ulaji. Usirudie vitu fulani fulani kila siku. Mathalan usiweke pilipili katika kila mlo. Tatizo ji...