Skip to main content

UGONJWA WA RETINA UNAOSABABISHWA NA KISUKARI



Jicho ni kiungo ambacho binadamu anapaswa kuwa makini kukilinda maana kuwapo kwake kunasaidia viungo kutenda kazi vyema.

idadi ya wagonjwa wengi wakisukari nchini na duniani inazidi kuongezeka. Ugonjwa huu wa macho huwapata watu wenye
kisukari cha muda mrefu.

Kuwapo kwa ugonjwa wa kisukari husababisha kuharibika kwa retina.

Hii ni sehemu ya nyuma ya jicho
ambayo inaundwa kwa utando wa neva ama mishipa ya fahamu.

Mishipa hii ya fahamu ni muhimu sana katika kumuwezesha mtu
kuona. Ndio inayopokea taswira ya vitu na kuipeleka katika ubongo kwa ajili ya tafsiri.

Kuathirika kwa neva hizi ni tatizo la hatari kwa uwezo wa jicho kuona kwani inaweza kusababisha kuwa na uwezo mdogo wa kutambua taswira ya vitu. Hali hii isipotibiwa
mapema, husababisha ulemavu wa kudumu.

Kisukari ni ugonjwa unaoingilia uwezo wa mwili kutumia na kuhifadhi sukari mwilini. Hii husababisha madhara makubwa mwilini. Sukari ndio nishati inayotegemewa na mwili katika kuendesha shughuli mbalimbali.

Kwa kawaida sukari katika mwili inatakiwa iwe katika kipimo cha saba hadi 12 (7-12).

Uwapo wa sukari nyingi katika
mzunguko wa damu husababisha madhara mbalimbali mwilini ikiwamo sehemu ya jicho ya nyuma
iitwayo retina.

Kadri sukari inavyozidi na muda unavyosogea, mfumo wa mzunguko wa damu katika jicho huathirika.

Ugonjwa hutokea pale sehemu ya retina inapokosa lishe kutoka kwenye vishipa vidogo
vinavyoathirika kutokana na wingi wa sukari mwilini.

Hali hii ikiendelea husababisha mishipa kuvujisha damu na maji maji hivyo kuzifanya tishu za retina
kuvimba na kuwapo na taswira yenye ukungu.

Tatizo hili huathiri macho yote
mawili na kadri mtu anavyoendelea kuugua kisukari ndivyo anavyokua
katika hatari ya kuathirika na
ugonjwa huu zaidi.

Dalili za ugonjwa huu Kuona ukungu au vidoadoa katika taswira unayotazama. Inawezekana pia akaona mawimbi wakati wa kutazama kitu, kushindwa kuona vizuri hasa nyakati za usiku, kuona
giza au kidoa katikati ya taswira imayoonekana.

Popular posts from this blog

TIBA YA MTU ALIEINGIWA NA JINNI SUGU.

kabla sijatoa tiba yake, ni lazima ujue unatibu nini na kwanini ni jinni. Maana zipo dalili mbalimbali zinazoonyesha mgonjwa amehusudiwa na jini na ni jini aina gani aliemuingilia muhusika. Zifuatazo ni aina na utaratibu wa kumtibu jini sugu. Dawa za kula. Habbatsaudai Habbatsufa Bakahadi Manimani Uzile Habbat rehani Karkam Halilinji Alhamza Kamun aswad Zamda Khardal Daarfilfil Filfil aswad Haltit Zaatar Harmal Sufa nyeupe Manimani Shomari Udinadi Ulinjani Sakabanji Kamun abyadh Uwatu Giligilani Karafuu Tangawizi Mdalasini Maua waridi Hakikisha dawa hizi umezitwanga na kuwa laini kisha utachukua kijiko kimoja cha kila dawa na kuchanganya kwenye asali safi ya nyuki lita moja na uisomee ruqya na mgonjwa awe anakunywa vijiko viwili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 30. NB Hakikisha wakati mgonjwa anatumia dawa za kula ambatanishe na za kujifukiza pamoja na za kujipaka. DAWA ZA KUFUKIZA kiribiti upele Sandarusi Haltit Karafuu maiti Mruturutu ...

KUONDOSHA MARADHI YA SUBIAN NA KUONDOA WASIWASI

Kwa mtu mwenye matatizo hayo achukue dawa zifuatazo :- - unga wa ambari nyeusi. - unga wa mvuje. - unga wa kitunguu thaum. - mafuta ya uto. - mafuta original ya zaituni. Maelezo Changanya na iwe unajipaka mwili mzima asubuhi na jioni kwa mda wa siku 21.

UTOSI KUINGIA NDANI KWA MTOTO MCHANGA.

chukua manjano mbichi iponde iwe laini sana, kisha chukua pamba na uiweke ile dawa, kisha muekee mtoto mchanga aliena tatizo hilo utosini. In shaa allah utosi utarudi sawa. Utafanya hivyo kwa siku mara moja mpaka tatizo litakapokwisha.