Skip to main content

TATIZO LA UPUNGUFU WA DAMU ( ANAEMIA ) KWA MAMA MJAMZITO.


Upungufu wa damu husababishwa
na nini?.


Upungufiu wa damu husababishwa na ukosefu wa madni chuma mwilini (Iron).


Mwili unaitaji madini chuma kwa wingi kwa ajili ya kutengeneza chembe hai nyekundu  za damu (red blood cell).


Unapokuwa mjamzito kiwngo cha madini chuma (Iron) yanayotakiwa mwilini huongezeka kutoka 18 milligram kwa siku mpaka 27 milligram kwa siku.


hii ni kutokana na mwili kuhitaji damu nying kwa ajili ya kufanya kazi mbalimbali zinazoongezeka mwilini kwa ajili ya kusapoti ukuaji wa mtoto.


Damu ni muhimu sana kwa mama
mjamzito.


Hivyo basi jitahid kula yakula vyenye kuongeza Damu.


Vyakula vinavyoongeza Damu
vimegawika katika makund mawili


Heme Iron.

hivi ni vyakula ambavyo mwili huweza kuichukua kirahis Iron yake navyo ni Nyama,Samaki,Kuku,Maini na Dagaa.


Pia kuna Non Heme.


hivi ni vyakula ambavyo vina Iron ya
kutosha ila mwil hauwezi kuichukua kirahis hivyo basi unapokula vyakula hivyo jitahid kula vyakula vyenye vitamin C kama Machungwa mapapai Nyanya na hoho ili usaidie kuchukuliwa kwake.


Mfano wa vyakula hivi ni Beetroot Mboga za majani zote hasa
matembele na spinach.Juice ya tembele na passion husaidia kuongeza damu kwa haraka hasa kwa wale ambao beetroot imewashinda,hii juice inaongeza damu kwa haraka sana


Njinsi ya kuandaa.


Osha matembele yako kwenye maji
ya vuguvugu kuondoa uchafu
ukimaliza yakate Kate weka kwa
blender na mbengu za passion
saga na maji,


ukimaliza chuja juice yako japo unaweza kunywa hivyo hivyo au ukaongezea sukari.


Unaweza changanya na ubuyu
mweupe pia badala ya passion
Ubuyu mweupe utatumia juice
yake Kunywa Mara mbili kwa siku kadri uezavyo ladha yake ni nzuri huwezi kushidwa tumia.


Vyakula vingine ni Mayai mayai
ya kienyeji Greenbeans.Maboga
Tambi Viazi vitamu.


Tende unaweza changanya na maziwa fresh Viazi mbatata au viazi ulaya Maharage viazi vitamu njegere ndegu Karanga almond Mbengu za maboga Kunde chemsha kunywa maji yake au supu yake.


Majani ya parachichi,chemsha
kunywa maji yake Unapokula vyakula vyenye Iron usinywe na chai kahawa au soya   huzuia (absorbtion)kuchukuliwa kwa madini chuma(Iron).


Pia unapokunywa vidonge vile vya
Damu ulivyopewa clinic baada ya
kumeza unatakiwa ule na Chungwa au Papai viweze kuchukuliwa mwilini kirahisi.


Dalili za kupungukiwa damu kwa
mama mjamzito.


Mama mjamzito unapohisi dalili
zifuatazo ni vizuri kupima wingi
wa damu,kwani kiasi cha damu
kinatakiwa kisiwe chini ya 11g/dL
mpaka mama unapoenda kujifungua

Kuchoka sana,japo kuchoka sana ni hali ya kawaida kwa mama mjamzito,hivyo unapoona unachoka sana ni vizuri kwenda kuangalia wingi wa damu.

kukosa pumzi (breathless).

Kizunguzungu,Maumivu makali ya kichwa.

Miguu kuishiwa nguvu.

Midomo kupauka.

kupata hamu ya kula udongo, ice
(mabarafu ) na vitu vyote
ambavyo sio vyakula.


Angalizo.

mama jitahidi kiwangu cha damu yako kiwe 11g/dL na kuendelea kipindi chote cha ujauzito kwani upungufu wa damu unaweza kusababishwa mtoto akazaliwa na uzito mdogo, kuzaliwa kabla ya muda.

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA FANGASI UKENI.

Fangasi ukeni ni muwasho sehemu ya ndani ya uke ambao unaweza kuambatana pia na kuvimba kwa uke. Leo sitaongelea sana juu ya nini kinasababisha hizi fangasi sehemu ya uke bali tutaona dozi kamili ya asili inayoweza kutibu kabisa tatizo hili linalosumbuwa wanawake wengi miaka sasa. Tumia dawa hizi 3 zote kwa pamoja ili kupata matokeo mazuri na usiache kuleta mrejesho hapa namna unavyoendelea: 1. LEMONADE Lemonade inaandaliwa kwa kutumia limau, maji, asali na mdalasini ya unga kidogo, nayo inaandaliwa hivi: *Chukua asali mbichi nusu Lita *Chukua limau kubwa 12 au zaidi, zikate katikati kila moja. Zikamuwe moja baada ya nyingine kupata maji maji ya limau mpaka umepata ujazo wa nusu lita. *Kwenye sufuria nyingine kubwa changanya mdalasini ya unga vijiko vikubwa 10 na maji lita 2 na nusu na uchemshe kama chai kisha ipua na uchuje na usubiri ipowe iwe ya uvuguvugu kidogo. *Sasa changanya pamoja asali nusu lita, juisi au maji maji ya limau nusu lita, maji ya uvuguvugu ya m...

TIBA YA MTU ALIEINGIWA NA JINNI SUGU.

kabla sijatoa tiba yake, ni lazima ujue unatibu nini na kwanini ni jinni. Maana zipo dalili mbalimbali zinazoonyesha mgonjwa amehusudiwa na jini na ni jini aina gani aliemuingilia muhusika. Zifuatazo ni aina na utaratibu wa kumtibu jini sugu. Dawa za kula. Habbatsaudai Habbatsufa Bakahadi Manimani Uzile Habbat rehani Karkam Halilinji Alhamza Kamun aswad Zamda Khardal Daarfilfil Filfil aswad Haltit Zaatar Harmal Sufa nyeupe Manimani Shomari Udinadi Ulinjani Sakabanji Kamun abyadh Uwatu Giligilani Karafuu Tangawizi Mdalasini Maua waridi Hakikisha dawa hizi umezitwanga na kuwa laini kisha utachukua kijiko kimoja cha kila dawa na kuchanganya kwenye asali safi ya nyuki lita moja na uisomee ruqya na mgonjwa awe anakunywa vijiko viwili mara tatu kwa siku kwa mda wa siku 30. NB Hakikisha wakati mgonjwa anatumia dawa za kula ambatanishe na za kujifukiza pamoja na za kujipaka. DAWA ZA KUFUKIZA kiribiti upele Sandarusi Haltit Karafuu maiti Mruturutu ...

KICHOMI

  Kichomi   ni moja ya dalili za ugonjwa moyo. Kupatwa kichomi mara moja moja si vibaya. Ukipatwa muda mrefu au kila wakati ; basi, chunguza zaidi. Kichomi husababishwa au kinaweza kuwa. Dalili ya matatizo ya tumbo lenye asidi (acid) kuzidi Dalili za ugonjwa wa moyo uitwao Ischemic Jambo la kuangalia ni je? Unashikwa kichomi ukiwa unatembea? Umeinama au umelala Ukishakula chakula Kama unapatwa kichomi wakati ukitembea au ukishafanya mazoezi makali ina maana kuna tatizo la damu kuingia sawasawa au kuzunguka (circulation) katika moyo. Kama unapatwa kichomi baada ya kula ina maana kuna tatizo katika chakula unachokula. Je mlo wako una acid(uchachu) sana? Je, unakula vyakula vyenye pilipili na binzari(spices) kwa wingi sana? Kama una kula sana vyakula vyenye asidi ina maana tumbo lako halimeng’enyui sawasawa linachoka. Kawaida binadamu unabidi kubadili badili ulaji. Usirudie vitu fulani fulani kila siku. Mathalan usiweke pilipili katika kila mlo. Tatizo ji...